I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, September 6, 2010

ZANZIBAR YAJENGA MATUMAINI KUPATA UANACHAMA WA FIFA

Naibu waziri kiongozi Ali Juma Shamhuna amesema juhudi za Zanzibar kupatiwa uwanachama wa shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA zimeanza kuleta matumaini baada ya kufunguliwa jalada rasmi la kuomba uanachama huo.

Shamhuna ambae pia ni waziri wa habari, utamaduni na michezo amesema rais wa FIFA Seif Blata ameahidi kulishughulikia ombi la Zanzibar la kupatiwa uwanachama wa shirikisho hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Zanzibar wakati akitokea Uswiss Shamhuna amezitaja baadhi ya hoja zilizowasilishwa kuomba uanachama huo ni kuwepo nchi ndogo nandi ya FIFA ambazo hadhi zake zinazidiwa na Zanzibar, huku zikiwa sio wanachama wa umoja wa mataifa.

Mwaka 2001 Zanzibar ilishindwa kupata uwanachama wa shirikisho hilo na mwaka huu ilianda hoja nzito za kuomba uanachama huo ambazo zinamwelekeo wa kuzaa matunda.

No comments:

Post a Comment