I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, September 26, 2010

MGOMBEA WA CUF MALIM SEIF AHADI KUCHIMBA MAFUTA NDANI YA KIPINDI CHA MIAKA MITANO

Chama cha wananchi CUF kimesema endapo kitaingia madarakani kuingoza Zanzibar suala la mafuta na gesi asilia litaondolewa kwenye orodha ya mambo ya muungano ndani ya kipindi cha miaka mitano.

Mgombea urais kupitia chama hicho Malim Seif Sharif Hamad amesema suala la mafuta na gesi asilia kuondolewa kwenye orodha ya mambo ya muungano halina lengo la kuvunja muungano bali ni kujali uchumi wa nchi ndogo na kubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari katika hoteli ya Ocean View mjini hapa amesema tayari baadhi ya makampuni yameonesha nia ya kutaka kuchimba mafuta yaliopo Zanzibar hivyo serikali yake itatakeleza suala hilo ndani ya kipindi cha miaka mitano.

No comments:

Post a Comment