I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, September 1, 2010

MGOMBEA URAIS WA ZANZIBAR KUPITIA CCM DR. SHEIN AREJESHA FOMU

Mgombea wa urais Zanzibar kupitia CCM Dr. Ali Mohammed Shein amesema ataitumikia Zanzibar kwa ufanisi mkubwa na kuweka mbele maslahi ya wananchi.

Akizungumza na wana CCM huko Kisiwandui muda mfupi baada kurudisha fomu za kuwania nafasi hiyo katika tume ya uchaguzi Zanzibar amesema atashirikiana vizuri na viongozi watakaokubali kufanyakazi kwa maslahi ya Zanzibar.

Aidha Dr. Shein ameonya kuwa hatamvumilia kiongozi yoyote ambae atakwenda kinyume na matakwa ya Wazanzibar endapo ataingia madarakani ……

Dr. Shein amesema katika uchaguzi ujao, CCM imejiandaa kuendesha kampeni za kistaarabu zenye kuwaelekeza wananchi malengo ya chama hicho ili wakipe ridhaa tena ya kuiongoza Zanzibar.

Nae naibu katibu mkuu wa CCM Zanzibar Saleh Ramadhan Ferouz amewataka wafuasi wa chama hiho kupuuza matamshi yanayotolewa na baadhi ya watu kwamba kumtilia kura kiongozi wa upinzani ni sawa na kumpigia mgombea wa CCM.

Amesema watu hao wanaopotosha wana CCM kwa kusambaza vipeperushi vyenye ujumbe huo, amewataka wafuasi wa chama hicho kuwa makini juu ya mbinu hizo zinazofanywa na vyama vya upinzani.

Dk . Shein anakuwa mgombea wa pili kurejesha fomu zake kwa tume ya uchaguzi Zanzibar kati ya wagombea wanane waliojitokeza kuchukua fomu za kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Octoba 31 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment