I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, September 1, 2010

MGOMBEA URAIS KUPITIA SAU ASHINDWA KUREJESHA FOMU

Ikiwa leo ni siku ya mwisho kurejesha fomu za kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar, mgombea wa nafasi hiyo kupitia Chama Cha Sauti ya Umma (SAU) Haji Mussa Kitole ameshindwa kurejesha fomu za kuwania nafasi hiyo kwa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).

Kitole awali alikataliwa kupewa fomu ya kuwania nafasi hiyo na ZEC kutokana na kuwa chama hicho kimetoa wagombea urais wawili wenye kutaka kuwania urais wa Zanzibar wakati sheria za ZEC zinaeleza chama kitowe mgombea mmoja wa nafasi hiyo.

Vyama ambavyo vimerejesha fomu leo katika afisi hiyo ni NCCR-MAGEUZI, TADEA, AFP, NRA, Jahazi Asilia huku chama cha SAU kikiwa bado hakijarejesha fomu hiyo.

Akizungumza na Zenji fm radio afisa wa habari wa tume ya uchaguzi Zanzibar Idriss Haji Jecha amesema hadi kufikia saa 9.45 cha cha SAU bado hakijarejesha fomu ambapo muda wa mwisho ulikuwa saa 10.00 jioni.

Amesema katika urejeshaji wa fomu hizo hakukuwa na kasoro zozote na fomu zilizorejeshwa zilikuwa safi.

SAU ndio chama pekee kilichoshindwa kuwasilisha fomu zake kwa tume ya uchaguzi ambapo vyama vyengine vilivyorejesha fomu zake jana ni pamoja Juma Ali Khatib (46) -TADEA, saa 4:13 asubuhi, Said Soud Said (62) AFP,saa 5:00, Haji Ambar Khamis (44) NCCR–Mageuzi, saa 5:30, Kassim Bakari Ali (43) Jahazi Asilia, saa 7.06, na Haji Khamis Haji (60) NRA saa 8:20 mchana.

Wengine waliorejesha fomu zao kwa ZEC wa mwanzo ni ni Mgombea wa chama cha wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ((67) alirejesha Agosti 16 majira ya saa 9:00 mchana wakati mgombea wa chama cha mapinduzi (CCM) Dk Ali Mohammed Shein (62) alijesha fomu yake Agosti 18 majira ya saa 8:30 mchana.

Akizungumza katika kikao hicho baada ya kupokea fomu hizo Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Khatib Mwinchande alisema kwao wao kujitokeza kwa wagombea wengi ni kupanuka kwa demokrasia nchini.

Mwenyekiti huyo aliwaomba wagombea wote ambao watateuliwa na tume kuingia katika mchakato wa kutaka urais baada ya kuhakikiwa fomu zao kuingia katika kampeni za kistaarabu zisizo na matusi ili kuepusha Zanzibar kuingia katika sura mbaya ya kukosekana amani.

Iwapo wagombea urais kutoka vyama hivyo hawatawekewa pingamizi uchaguzi mkuu kwa nafasi ya urais unatarajiwa kufanyika Octoba 31 mwaka huu utakuwa na wagombea saba

No comments:

Post a Comment