I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, September 1, 2010

MAELFU YA WAUMINI WA KISLAMU WAMZIKA MUFTI MKUU WA ZANZIBAR

Maelfu ya waumini wa dini ya kislamu na wananchi wengine leo wamehudhuria maziko ya mufti mkuu wa Zanzibar sheikh Harith bin Helf aliefariki nchini India Alhamis iliyopita.

Maziko hayo yaliofanyika kijijini kwao Muyuni Wilaya ya Kusini yameongozwa na makamo wa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. Ali Mohammed Shein.

Viongozi wengine waliohudhuria maziko hayo ni rais mstaafu wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi, waziri kiongozi wa Zanzibar Shamsi Vuai Nahodha na mufti mkuu wa Tanzania bara Sheikh Shaaban bin Simba na viongozi wengine wa serikali na kidini.

Marehemu Harith amezaliwa mwaka 1927 katika kijiji cha Muyuni alipata elimu ya msingi mwaka 1937 na elimu ya chuo kikuu cha Alzhar nchini Misri na kuchaguliwa mufti mkuu wa Zanzibar mwaka 1992.

Marehemu alifariki dunia nchini India katika hospitali ya Miyot alikukuwa akitibiwa ugonjwa wa moyo na uti wa mgongo. Mungu ailaze roho ya marehemu peponi amina.

No comments:

Post a Comment