I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, September 1, 2010

CHADEMA YATAKA RAIS KIKWETE AWEKEWE PINGAMIZI

Chama cha Demokraisa na maendeleo CHADEMA kimewasilisha malalamiko kwa msajili wa vyama vya siasa kikitaka mgombea wa urais wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM rais Jakaya Kikwete awekewe pingamizi katika kinyanganyiro cha uchaguzi wa urais.

Hoja kuu ya CHADEMA kuweka pingamizi ni kwa serikali kupandisha mishahara ya wafanyakazi waliokusudia kugoma wakati wa mkutano wa uchumi wa dunia, lakini rais Kikwete wakati huo alisema hawezikupandisha mishahara.

Kaimu katibu mkuu wa CHADEMA John Mnyika amesema hatua ya sasa ya serikali kupandisha mishahara ya watumishi wa umma inahesabiwa kama yenye kutaka ungwaji mkono na wafanyakazi.

Mnyika amedai suala la nyongeza wa mishahara kwa wafanyakazi halikuongezwa na bunge kama vile ilivyopendekezwa hivyo suala hilo linatumiwa kama kampeni za mgombea huyo na kwenda kinyume na sherria ya gharama za uchaguzi

No comments:

Post a Comment