I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, September 1, 2010

CHADEMA KUMUWEKEA PINGAMIZI RAIS KIKWETE

Kaimu katibu mkuu wa chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA John Mnyika amesema chama hicho kinaendelea na taratibu zake katika afisi ya msajili wa vyama vya siasa na tume ya uchaguzi ya taifa kupinga kile alichodai mgombea wa urais kupitia CCM rais Jakaya Kikwete kukiuka sheria ya uchaguzi ya mwaka 2010.

` Wakati CHADEMA ikiendelea na harakati hizo naibu katibu mkuu wa CCM Tanzania Bara Peuce Msekwa amesema mgombea huyo hajavunja kifungu chochote cha sheria na inasubiri suala hilo liwasilishwe katika afisi husika ili itowe utetezi wake.

Vyombo vya habari vimeripoti kuwa mgombea urais wa wa CHADEMA Dr. Wilbord Slaa amepanga kuwasilisha pingamizi kwa msajili wa vyama vya sisasa nchini John Tendwa kwa madai mgombea urais wa CCM rais Jakaya Kikwete amevunja kifungu nambari 21 cha sehria ya gharama za uchaguzi.

No comments:

Post a Comment