I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, September 6, 2010

BIDHAA MBOVU ZIMEZAGAA ZANZIBAR

Bidhaa zilizopitwa na viwango zimeanza kuzagaa katika kipindi hichi cha kumalizia mwezi mtukufu wa ramadhani ambazo huuzwa kwa bei nafuu.

Wananchi wametakiwa kuchukua tahadhari kutokana na uingizaji wa bidhaa mbovu ulioshamiri hapa Zanzibar hasa kipindi hiki cha kukaribia siku kuu ya Edil fitr.

Hatua hiyo imekuja kufuatiwa kuwepo kwa wimbi kubwa la uingizaji wa vyakula vilivyopita na muda wa matumizi ya binadamu ambalo limezuwa malalamiko kutoka kwa wananchi

Uchunguzi uliofanywa na Zenji Fm radio leo na jana umegundua mchele mbovu aina ya Busmat wenye ujazo wa kilo tano ukiuzwa kwa shilingi elfu sita na tano katika maeneo ya Darajani mjini Zanzibar.

Mchele huo unaouzwa na wafanyabiashara za mikononi maarufu wamachinga unaonesha kutengenezwa March 2008 na kumaliza muda wa matumizi March 2011 ni mbovu na unatoa harufu mbaya unapofunguliwa.

Akizungumza na zenji Fm radio juu ya malalamiko hayo mrajisi wa bodi ya chakula, dawa na vipodozi Dr. Burhan Simai amesema bodi hiyo haina sheria ya kuwadhibiti wafanyabiashara wanaojulikana wamachinga.

Hata hivyo amesema bodi hiyo inafanya ukaguzi katika sehemu zote zinazoingizwa bidhaa Unguja na Pemba na kukagua makontena yote ya bidhaa

Hivi karibuni hiyo imekamata tani 245 za mtama na tani 193 za mchele kutoka nje ya nchi zikiwa zimeharibika na havifai kwa matumizi ya binadamu.

Kutokana na hali hio Dk Simai aliwataka wananchi kuchukua tahadhari wakati wanaponunu

No comments:

Post a Comment