I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, April 28, 2010

ZSSF WAJIBU CHAMA CHA WAFANYAKAZI ZNZ

Mfuko wa hifadhi ya jamii Zanzibar ZSSF umesema sababu zilizochangia kuchelewa kutoa mafao ya uzazi na mafao ya matibabu ni kutokana na mfuko huo kuwa na uhaba wa raslimali zake .
Akizungumza na zenji Fm Radio afisa uhusiano wa mfuko huo Mussa Yussuf amesema uamuzi huo umetolewa baada ya wataalamu kutoka shirika la kazi ulimwenguni ILO Kufanya tathmini ya uwezo wa mfuko huo na wameishauri serikali kusitisha utoaji wa mafao hayo ili kuunusuru mfuko huo kufilisika.
Amesema kutokana na hali hiyo waziri anaehusika na fedha na uchumi ambae kwa mujibu wa sheria ya mfuko huo anauwezo wa kusitisha kutoa mafao hayo…
Afisa huyo ametoa ufafanuzi huo kutokana na madai yaliyotolewa na katibu mkuu wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi Zanzibar Zatuc Khamis Mwinyi akidai kusikitishwa na uchelewaji wa kutolewa kwa mafao ya uzazi na matibabu na mfuko huo.

No comments:

Post a Comment