I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, April 12, 2010

WAZIRI KIONGOZI AMESEMA MATATIZO YA MUNGANO KATIKA SEKTA ZA FEDHA NA BIASHARA YANAHITAJI MFUMO MAALUM


Waziri kiongozi wa serikali ya Mapinduzi Zaznibar Shamsi Vuai Nahodha amesema matatizo ya mungano katika sekta za fedha na biashara yanahitaji mfumo maalum wa utatuzi wake ili kuleta maslahi kwa pande mbili za muungano
Amesema licha tume ya pamoja ya fedha ya Muungano kuwasilisha ripoti yake kwa serikali zote mbili ya mgawanyo wa mapato, lakini hatua hiyo itasaidia kutatua tatizo hilo kwa asilimia 60.
Waziri kiongozi Nahodha amesema katika mahojiano maalum na redio Uhuru huko afisini kwake.
Kuhusu hali ya baadae ya Zanzibar itavyofaidika na Soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki amesema bado itakabiliwa na changamoto za kitaalamu na mitaji ambazo zinaweza kukwamisha biashara za Wazanzibari.
Hata hivyo, amesema Zanzibar inaweza kufaidika kama itakuwa na viwanda vidogo vidogo vya samaki na maabara za kuchunguza bidhaa hizo zitazosafirishwa nje ya Jumuiya hiyo.

No comments:

Post a Comment