I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, April 14, 2010

WALIO VUNJIWA NYUMBA ZAO KWARARA WAIJIA JUU SERIKALI


Baada ya takriban mwaka mzima kupita
tokea wananchi wa eneo la Kwarara kubomolewa nyumba zao. Baadhi ya wananchi hao leo wamejitokeza katika kituo cha Zenj fm Radio na kutoa malalamiko yao.
Akizungumza na Mwangaza wa Habari Mwenyekiti wa kamati ya waliovunjiwa Bw Khamis Hassan Ali amesema kuwa kuna baadhi ya viongozi wanawalazimisha kuondoka katika maeneo hayo wakati maeneo hayo kesi yake bado iko mahakamani na haijatolewa uamuzi wowote
Aidha ameiomba serikali kulifuatilia kwa kina suala hilo ili wananchi wapatiwe haki zao.
Lakini katika hali ya kushangaza Bw Khamis Hassan Ali amedai kuwa kuna baadhi ya viongozi wanaowalazimisha wananchi hao kuhama ambapo amemtaja Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Fedha na Uchumi) wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dr Mwinyihaji Makame…bonyeza HAPA kumsikia Bw Khamis Hassan Ali...Mwenyekiti wa kamati ya waliovunjika

Nae mkaazi wa Kwarara Bw Ali Khamis Hassan ameungana na mwenyekiti wa kamati hiyo ya waliovunjiwa kwa kusema kuwa wamevunjiwa nyumba zao kwa uonevu mkubwa huku wakiishi katika mazingira ya kusikitisha.
Katika malalamiko yake Bw Ali Khamis Hassan amesema kuwa wameshangazwa na kitendo cha sheha wa shehia hiyo pamoja na viongozi wengine kutembelea eneo linalomilikiwa na wananchi hao ambapo kwa mujibu wa Bw Ali,eneo lililotembelewa linataka kujengwa skuli. Aidha ameiomba serikali kuchukua hatua za haraka kulipatia ufumbuzi suala hilo kabla amani haijavunjika.…Bonyeza HAPA kumsikia Bw Ali Khamis Hassan...Mkaazi wa Kwarara

Akimalizia malalamiko yao Bw Salum Seif Salum ambae pia ni mjumbe wa kamati ya watu waliovunjiwa na mkaazi wa Kwarara ameelekeza malalamiko yake kwa baadhi ya viongozi wa ngazi za juu serikalini na kumuomba Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mh Aman Abeid Karume kuwashuhulikia viongozi aliowateua katika ngazi mbali mbali kwa vile ndio wa kulaumiwa kutokana na ubinafsi wao katika majukumu aliyowakabidhi.
Bw Salum pia ameelekeza malalamiko yake kwa baadhi ya taasisi za kutetea haki za binadamu na wasomi mbali mbali waliopo nchini kwa madai kuwa wameshindwa kutetea maslahi ya wanyonge waliovunjiwa maeneo ya Kwarara…Bonyeza HAPA kumsika Salum Seif Salum...mjumbe wa kamati ya watu waliovunjiwa Kwarara

Baada ya kuwasikia wananchi hao wakilalamikia kitendo cha baadhi ya viongozi kuchukua eneo hilo,Mwangaza wa Habari ulifanya juhudi za kumtafuta Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Fedha na Uchumi), Dk. Mwinyihaji Makame Mwadini,ambae yeye amesema kuwa si kweli kuwa amechukua eneo hili kwa vile yeye hana uwezo wa kuchukua ardhi wala hana mamlaka hayo Bonyeza HAPA kusikia majibu ya sakata lote kutoka kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Fedha na Uchumi), Dk. Mwinyihaji Makame

No comments:

Post a Comment