I made this widget at MyFlashFetish.com.

Saturday, April 24, 2010

VYAMA VIDOGO VYA SIASA ZANZIBAR VYATISHIA KUJITOA KWENYE UCHAGUZI 2010

Chama cha siasa cha NLD kimeanza kuvishawishi vyama vingine vidogo vya siasa kususia uchaguzi mkuu wa Zanzibar kutokana na tume ya uchaguzi kutangaza viwango vikubwa vya fedha za dhamana kwa wagombea wa vyama watakaoshiriki katika uchaguzi huo.

Akizungumza na Zenji Fm Radio juu ya taarifa hiyo ya tume iliyotolewa kwenye vyombo vya habari naibu katibu mkuu wa NLD Zanzibar Rashid Ahmmed amesema uwamuzi huo utawafanya matajiri kutumia fedha zao kushiriki kugombea nafasi za uongozi na kuwacha wale wasiokuwa na uwezo wa kifedha.

Amesema chama cha NLD kinapinga viwango vya fedha za dhamana vilivyotangazwa na tume kwa vile havitoi fursa kwa wagombea wa vyama vidogo ambavyo havina ruzuku kushiriki katika uchaguzi huo wa demokrasia.

Bw. Ahmmed amesema tangazo hilo la tume ya uchaguzi litalipa nafasi zaidi vyama vinavyopewa ruzuku na serikali ambavyo ni CCM, CUF na CHADEMA na kusema hatua hiyo sio demokrasi ya vyama vingi…

Aidha naibu katibu mkuu huyo wa NLD amesema pamoja na tume ya uchaguzi haiwezi kushtakiwa kisheria, lakini wananchi wenyewe ndio watakaofanya maamuzi juu ya taarifa ya tume hiyo ya kuongeza viwango vya dhamana kwa wagombea wa urais, uwakilishi na udiwani.

Jana tume ya uchaguzi Zanzibar iltoa taarifa ya kupandisha dhamana kwa wagombea wa kiti cha urais wa Zanzibar kutoka shilingi milioni moja hadi milioni tatu, nafasi ya uwakilishi kutoka elfu 50 hadi laki tatu na udiwani kutoka elfu 15 elfu 50.

Akizungumza na Zenji Fm radio afisa habari wa tume hiyo Idriss Haji Jecha amesema kiwango hicho kimeongezwa kutokana na hali ya kifedha ya watu wanaotaka kugombania urais na kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania.

Uchaguzi mkuu wa Zanzibar utakaomchagua rais, wawakilishi na madiwani unatarajiwa kufanyika tarehe 31 Octoba na matokeo yake yanatarajiwa kutangazwa siku hiyo hadi tarehe pili Octoba mwaka huu

No comments:

Post a Comment