I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, April 26, 2010

ULIPAJI WA KODI BADO NI TATIZO ZANZIBAR


Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imesema bado tatizo la wafanya baishara wa Zanzibar kutozwa kodi mara mbili wanaposafirisha bidhaa zao Tanzania bara halijapatiwa ufumbuzi kutokana udhaifu wa watendaji.
Akizungumza na Zenji Fm radio juu ya mafanikio ya miaka 46 ya Muungano wa Tanganyika na Zanizbar waziri wa nchi afisi ya waziri kiongozi Hamza Hassan Juma amesema serikali inasikitishwa na tatizo hilo kwa vile imekuwa ikitoa maagizo, lakini utekelezaji wake ni mdogo.
Amesema anashangazwa na mizigo inayopiliwa ushuru Tanzania bara na inapukuja Zanzibar hailipiwi ushuru tena, lakini hali hiyo inakuwa tofauti na mizigo ya biashara inayokwenda Tanzania bara ambayo pia hukwama kwa siku kadhaa…Bonyeza hapa kumsikia Bwana -HAMZA
Waziri Hamza amesema serikali inafahamu TRA ni moja ya taasisi inayokusanya mapato ya Zanzibar yanayoingia katika mfuko mkuu wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar, lakini upande wa Tanzania bara taasisi hiyo haiwetendei haki wafanyabiashara wa Zanzibar.

Hata hivyo amesema katika kikao kilichomalizika hivi karibuni serikali ilitoa agizo kwa maafisa wa Zanzibar kukaa pamoja na maafisa wa TRA Tanzania bara ili kulipatia ufumbuzi tatizo hilo.
Aidha waziri Juma amesema suala hilo pia linatarajiwa kuzungumzwa katika kikao cha mawaziri wa Zanzibar na Tanzania kitakachofanyika tarehe tatu mwezi ujao na baade kuitishwa kikao cha kero za muungano…..CLIPS…… KODI
Tatizo la wafanyabiashara wa Zanzibar kutozwa kodi mara mbili wakati wanapopeleka bidhaa zao Tanzania bara limekuwa la muda mrefu na kuleta usumbufu kwa wafanyabiashara hao.

No comments:

Post a Comment