I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, April 15, 2010

TUME IMEKATAA KURUDIA UWANDIKISHAJI ZANZIBAR


Tume ya uchaguzi Zanzibar imesema haina mpango wa kurudia aundikishaji wa wananchi katika daftari la wapiga kura licha ya idadi ndogo ya watu waliosajiliwa katika baadhi ya maeneo.
Akizungumza na Zenji Fm radio mkurugenzi wa tume hiyo Salum Kassim Ali amesema bado tume hiyo haijapanga uandikishaji mwengine baada ya kumalizika uandikishaji wa awamu ya pili
Amesema licha ya kuwepo malalamiko ya watu kunyimwa haki zao katika uandikishaji huo, lakini malalamiko hayo ni machache ikilinganishwa na uchaguzi uliopita baada ya tume hiyo kuvishirikisha vyama vya siasa kuangalia shughuli za undikishaji.
Amesema uandikishaji wa awamu ya pili unatarajiwa kumalizika Mei mwaka huu na tume ya uchaguzi inaendelea na maandalizi ya upigaji kura kwa kutoa vitambulisho kwa kila aliejindikisha katika daftari la wapiga kura.
Aidha bw. Kassim amesema mipango ya uteuzi wa wagombea na elimu ya wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi huo imekamilika na maandalizi mingene yanakwenda vizuri.

No comments:

Post a Comment