I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, April 27, 2010

SAKATA LA ZATUC

Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Zanzibar ZATUC linakusudia kuwashawishi wanachama wao kutochangia mfuko wa hifadhi ya jamii Zanzibar ZSSF kutokana na mfuko huo kutotimiza ahadi katika utoaji wa mafao ya uzazi na ugonjwa kwa wananchama wake.
Akizungumza na zenji fm radio katibu mkuu wa ZATUC Khamis Mwinyi Mohammed amesema mfuko huo kwa muda mrefu sasa umeshindwa kutoa mafao hayo huku ukiendelea kuwachanganisha wanachama wake.
Amesema kwa vile shirikisho lao lina mjumbe katika bodi ya ZSSF wanafikiria kumtoa mjumbe huyo ili kuepuka kushirikishwa katika mpango huo wa ZSSF unaokwenda kinyume na sheria za kuanzishwa kwa mfuko huo kwa kukosa kulipa mafao hayo
Mfuko wa ZSSF ulioanzishwa mwaka 1998 hivi unaendelea kutoa mafao ya uzeeni kwa wananchama wake wanaostaafu kazi.

No comments:

Post a Comment