I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, April 12, 2010

RAIS WA ZANZIBAR DR. AMANI ABEID KARUME AMETUMA SALAMU ZA RAMBI RAMBI KUFUATIA KIFO CHA RAIS WA POLAND


Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dr. amani Abeid Karume ametuma salamu za rambi rambi kufuatia kifo cha rais Lech Kaczynski wa Poland baada ya ndege aliyokuwa akisafiria kuanguka nchini Urusi ikiwa na zaidi ya abiria 90 akiwemo mkewe.
Katika salamu hizo Dr. Karume ameelezea masikitiko yake na kushtushwa na kifo hicho pamoja na maafisa wengine wa serikali ya Poland waliokuwemo kwenye ndege hiyo.
Rais Karume ametuma salamu hizo kwa kaimu rais wa nchi hiyo pamoja na raia wa Poland.
Amesema wananchi wa Zanzibar wanaungana na wenzao wa Poland katika maombelezi ya msiba huo na kusema uhusiano wa nchi mbili hizo utaendelezwa zaidi

No comments:

Post a Comment