I made this widget at MyFlashFetish.com.

Friday, April 9, 2010

RAIS JAKAYA KIKWETE AMEWAONYA BAADHI YA VIONGOZI WA CHAMA HICHO KWA KUANZA KAMPENI ZISIZO RASMI KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU UJAO.


Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM rais Jakaya Kikwete amewaonya baadhi ya viongozi wa chama hicho kwa kuanza kampeni zisizo rasmi kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao.
Rais Kikwete amesema kampeni hizo zinavunja kanuni na katiba ya CCM ambayo inahimiza ustawi wa demokrasia ndani ya chama na nchi.
Rais Kikwete amesema hayo katika ufunguzi wa semina kwa viongozi wandamizi wa chama hicho mjini Dar es Salaam katika ukumbi wa Karimjee.
Mwenyekiti huyo amesema vitendo vya aina hiyo vinaweza kuleta mgawanyiko miongoni mwa wafuasi wa chama hicho na ndani ya chama chenyewe.
Katika kutekeleza mkakati mpya ndani ya CCM, chama hicho kitatumia utaratibu mpya wa kuwapata wagombea wa uchaguzi mkuu badala ya utaratibu wa zamani.

No comments:

Post a Comment