I made this widget at MyFlashFetish.com.

Friday, April 9, 2010

MWALIMU ‘FATAKI’ AVURUGA MABINTI SKULI YA VIKOKOTONI .AMKATISHA MASOMO BINTI KIDATO CHA TATU

SASA imedhihirika kwamba Mwalimu wa Sekondari ya Vikokotoni mjini hapa, ni kitangi au fataki baaada ya kuooa mwanafunzi wa kidato cha tatu wa skuli huyo, mwenye umri wa miaka 16.

Habari za uhakika kutoka vyanzo mbalimbali, vinasema kwamba mwanafunzi huyo aliyegeuzwa mke, anaitwa Safia na mwalimu huyo, Fadhili Mkali, amejitetea kuwa aliona binti wa nyumbani.

Mzazi wa mtoto huyo, alilithibitishia NIPE HABARI, kwamba: “Nimeozesha binti yangu,” baada ya msichana huyo kwenda kumshataki kwa kadhi juu ya suala hilo .

Mzazi huyo ambaye kwa sasa aliomba kutotambulishwa gazetini, alisema: “Nimeamua kuozesha baada ya kushindwa kwa watu wote kumshawishi binti kuacha kuolewa. Ilishindikana kabisa.”

“Wajomba zake na shangazi zake na watu wote wamekataliwa na tukaamua kumuozesha, lakini bado yuko nyumbani kwa kisingizio cha kumaliza mambo yao . Bado hajamchukua,” alisema baba huyo aliyeozesha juzi Jumatano.

“Niliona bughuza kunifikisha kwa kadhi kunishitaki,” alisema mzee huyo aliyekuwa na hali ya mashaka na wasiwasi wakati angongea na mwandishi wetu.

Akizungumza na Zenjfm , kama atakubali msaada sheria ili mtoto huyo andelee na masomo, alisema hana haki ya kumrithi kwa walivyokubaliana na mtoto wake huyo baada ya kumfungisha ndoa.

Akisimulia kuhusu suala hilo , mama mzazi wa mwanafunzi huyo, alisema: “Baada ya hali kuwa mbaya, Safia alikuwa hasemi na mtu humu ndani.”

Alisema kuwa mwalimu huyo alikuja yeye na kusema kuwa anataka kuolewa na huyo kijana ambaye inaelezwa kuwa amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na baadhi ya wanafunzi.

Mama huyo ametoa wito kwa wazazi wengine kuwa makini na mabinti zao kwake wa kwake, ilishindikana baada ya kutaka kuolewa na mwalimu huyo.

Mjomba wa mtoto huyo, ambaye pia aliombwa asitambulishwe kwa jina gazetini, alisema: “Sisi tunamwambia tunahitaji msaada kwani mwalimu huyu ana kesi tatu kwa watoto tofauti kwani sisi wizara ya elimu ilishindwa kutusadia badaa ya sisi kwenda wizara ya bila ya msaada wowote mpaka sasa.”

Mwenyekiti wa kamati ya skuli ya Vikokotoni, alithibitisha kuolewa kwa binti huyo akisema: “Suala hili tumelipokea na sasa tunakutana ili kulifanyia uamuzi wa jambo hilo ,” alisema na kukata simu.

Bi. Mwamidi kutoka Wizara ya Elimu, alisema wamepokea kesi hiyo kwa ajili ya kushughulikia katika misingi ya ushauri na malezi.

Alithibitisha kuwa mwalimu huyo walimwita na kufanya mahojiano na akajibu alimkuta nje ya geti la shule na kumwambia juu ya kutaka kumuoa na kwamba hakudhani kama mwanafunzi.

Wizara ya elimu ilipendekza kuwa mwalimu apewe onyo na kupewa uhamisho.

Wakati huo wizara ya elimu imethibitisha kuwa wakati inashulikia jambo hilo tayari kuna kesi mbili hazijashughulikiwa zinazomuhusu mwalimu huyo juu ya uhusiano wa kimepanzi na mwalimu.

No comments:

Post a Comment