I made this widget at MyFlashFetish.com.

Friday, April 16, 2010

MWAKILISHI WA JIMBO LA TUMBE CUF AMTWANGA NGUMI MUUZA SAMAKI

Mwakilishi wa jimbo la Tumbe CUF,Ali Mohd Bakar huenda akafikishwa mahakani baada ya kumtwanga ngumi mchuuzi wa samaki kisa ni kudondokewa na tone la maji ya mavumba ya samaki katika gari ya abiria waliokuwa wakisafiria

Tukio hilko lilitokea juzi majira ya saa tano asubuhi huko Wingwi wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Kadhia hiyo ya aina yake ilitokea wakati wa msafara huo ambapo mchuuzi huyo Said Kombo mkaazi wa Wete alipokuwa akisafirisha biashara yake hiyo.
Akisimulia tukio hilo Bw Kombo amesema kuwa mheshimiwa huyo alimtolea maneno ya kashfa baada ya maji hayo ya mavumba kumdondokea kwa bahati mbaya na baada ya majibizano kutokana na kitendo kile aliamua kumpiga ngumi.
“Baada ya kudondokewa na maji hayo tukasimamisha gari akaenda kujisafisha lakini hatimae baada ya kurudi ndani ya gari mie nikaenda kukaa kule kulikochafuka na mimi lakini bwana huyo hakuridhika akaanza kunitolea maneno machafu,mjinga wewe,mwanaharamu,mshenzi na akaniambia kuwa vumba lako likiniingia tena nitawaangusha samaki wako,mimi kwa vile ni binadamu niakapandwa na hasira nikamwambia huwezi baada ya kumwambia hivyo akanipiga ngumi,mimi nikamuuliza je bwana mkubwa umeridhika akaniambia ndio nishakupiga na kashtaki popote”

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa Kaskazini Pemba Yahya Rashid Bugi amesema kuwa kesi hiyo ilifikishwa kituo cha polisi tarehe 12 mwezi huu.
Aidha kamanda bugi amesema kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea ambapo Bw Soud ametakiwa kupeleka mashahidi wake ili kesi hiyo ipelekwe mahakamani.

No comments:

Post a Comment