I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, April 29, 2010

MVUA ZA MASIKA ZALETA MAFURIKO DAR MTU MMOJA AFARIKI DUNIA


Madhara ya mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbali mbali nchini ikiwemo mjini Dar es Salaam yameendelea kuwakumba wakaazi wa mji huo ambapo baadhi ya miundo mbinu imesombwa na maji huku baadhi ya watu hawajulikani walipo.

Mvua hizo zimekuwa zikinyesha kwa siku tatu mfululizo zimesababiosha kifo cha mtu mmoja mkaazi wa Temeke na kusababisha usumbufu kwa watumiaji wa barabara kutokana na baaadhi ya barabara kujaa maji na kusababisha msongomano wa gari.

Aidha mvua hizo zimesababisha kusombwa baadhi ya madaraja.

Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya hali ya hewa Tanzania Dr. Arnest Kijazi amesema mvua hizo zinazoendelea kunyesha katika ukanda wa pwani ya Tanzania zitaendelea hadi mwisho mwa mwezi huu.

Dr. Kijazi amewataka wakaazi wa maeneo hayo kuchukua hatua za tahadhari

No comments:

Post a Comment