I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, April 26, 2010

MATATIZO YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR YANATOA CHANGAMOTO YA KUIMARISHA MUUNGANO HUO ZAIDI.


Waziri wa mawasiliano na uchukuzi Zanzibar Brigedia mstaafu Adam Mwakanjuki amesema matatizo ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar yanatoa changamoto ya kuimarisha muungano huo zaidi.
Akizungumza na Zenji fm radio juu ya mafanikio ya miaka 46 ya muungano amesema matatizo hayo yanaweza kuondoshwa na watanzania wenyewe hatua kwa hatua baada ya kulaumiana kwa kila upande.
Amesema muungano wa Tanzania ni wakupigiwa mfano katika nchi nyingi duniani zilizoungana ambapo hivi sasa muungano huo haupo tena, hivyo ni vyema kwa watanzania kuendelea kuudumisha muungano wao...Bonyeza hapa kumsikia Brigedia mstaafu Adam Mwakanjuki
Aidha waziri Mwakanjuki amesema haja ya kuwepo muungano ipo na kuwataka wale wanaokosoa kupelekea agenda zao katika kamati maalum baada ya kuendelea kulalamika.
Waziri Mwakanjuki ambae hajaonekana hadharani kwa miezi kadhaa yuko katika likizo ya ugonjwa baada ya kupata ajali mkoani Dodoma akiwa katika majukumu ya kutekeleza shughuli za chama tawala cha CCM.

No comments:

Post a Comment