I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, April 13, 2010

MAKAMBA...AJIBU SHUTUMA ZA WAPINZANI JUU YA KUKUSANYA MABILIONI


Chama cha Mapinduzi CCM tarehe 8 April mwaka huu kulizindua kampeni ya uzinduzi wa kukichagia chama hicho kwa njia ya jumbe mfupi wa simu (SMS) ambapo chama hicho kinategemea kukusanya shilingi bilioni 50.
Kufuatia hatua hiyo amabyo imetiliwa shaka na baadhi ya vyama vya siasa kikiwemo cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kwa mujibu wa gazeti la Tanzania Daima la aprili 1 mwaka huu.
Kwa mujibu wa gazeti hilo Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, aliielezea hatua hiyo ya CCM kuwa ni kielelezo cha namna chama hicho tawala kilivyo mstari wa mbele kuvunja Sheria ya Gharama za Uchaguzi iliyosainiwa kwa mbwembwe na Rais Jakaya Kikwete hivi karibuni.
Ukiachana na CHADEMA, chama cha wananchi CUF nacho kimeungana na CHADEMA ambapo wamedai kuwa hatua hiyo ni uvunjifu wa sheria ya gharama za uchaguzi iliyosainiwa na Rais Kikwete. Chama cha CUF kimedai kuwa hawaamini kuwa CCM ina uwezo wa kuchagisha milioni 40 kutoka kwa wanachama wake wa kawaida na badala yake fedha hizo zitapatikana kupitia kwa wafanyabiashara ambao wanatumia fedha zao kwa maslahi yao binafsi bonyeza hapa kumsikia Bw JUMA DUNI

Kufuatia madai hayo Mwangaza wa Habari ulimtafuta Katibu Mkuu wa CCM,Bw Yussuf Makamba ambapo alipoulizwa juu ya hilo alijibu kama ifuatavyo bonyeza hapa kumsikia MAKAMBA

No comments:

Post a Comment