I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, April 15, 2010

IDADI YA WATALII IMEPUNGUA ZANZIBAR


Idadi ya watalii wanaoitembela Zanzibar imepungua kwa kwa kiasi kikubwa kuanzia March mwaka huu, hali ambayo inatishia kupungua nafasi za ajira katika sekta ya utalii.
Akizungumza na Zenji Fm radio mwenyekiti wa Jumuiya ya wawekezaji wa utalii Zanzibar Simai Mohamed Said amesema hali hiyo ni ya kawaida inayotokea katika kipindi cha mwezi wa March hadi April kila mwaka.
Hata hivyo amesema kukatika kwa huduma ya umeme kwa kipindi cha miezi mitatu na mgogoro wa kiuchumi duniani pia imepunguza idadi ya watalii wanaotembelea Zanzibar.
Amesema katika kukabiliana na hali hiyo jumuiya ya wawekezaji wa sekta ya utalii Zanzibar inaendelea kutoa taarifa kwa mashirika ya kimataifa ya waongozaji wa wageni

No comments:

Post a Comment